Bagamoyo
ni mji ulioanzishwa mwishoni mwa karne ya 18. Ukiwa kama mji mkuu wa Wajerumani
Afrika Mashariki, mji ulio kua na bandari kubwa na biashara nyingi wakati ule.
Hapo
awali kabla yakufikia karne ya 18, bagamoyo ilikua ni kituo kidogo cha biashara
mbalimbali ikiwemo samaki, chumvi na gundi. wakazi wake wengi walikua ni wavuvi
wa samaki na wakulima.
Katika
karne ya 19, waarabu waliwasili na kupageuza kua kitovu cha biashara ya utumwa
kwa Afrika Mashariki. Hii ilipoteza sifa yake iliokua nayo kwa kiasi
kikubwa kwani walipageuza kua ndio kituo cha misafara ya watumwa kutoka katika
ya nchi.
Mwishoni
mwa karne ya 18 familia 12 za kiislam ziliweka makazi katika mji wa bagamoyo
wakiwa wote ndugu wa Shamvi La Magimba kutoka Oman. walio ishi kwa
kulazimisha makusanyo ya kodi kwa watu hata kwenye mambo kama kuchinja
mbuzi au kuvua samaki, na biashara ya chumvi, ambayo ilikua inafanyikia vijiji
vya Nunge, umbali wa KM 3 kaskazini mwa Bagamoyo.
Watumwa
walikua wakiwekwa katika magereza na inapofika usiku, walikua wakisafirishwa
kwa meli katika soko la wa tumwa mjini Zanzibari. Hii ilitengeneza maana ya
jina BAGAMOYO(Bwaga-Moyo). Kwamba wale walio kua wakisafirishwa kutoka Bagamoyo
walikua hawarudi tena nyumbani kwao.
![]() |
sanamu zikionyesha jinsi gani watumwa walikua wanafungwa wakisubiri kusafirishwa kwenda kuuzwa zanzibari. |
Mwaka
1868: kulianzishwa kwa misheni ya kikatoliki
Katika
mwaka 1868, watawala wadogo mjini Bagamoyo walio julikana kama wajumbe,
waliwasilisha misheni (dini) ya kikatoliki (mababa wa roho mtakatifu) jambo
lililoleta upinzani kutoka kwa watu wenye asili ya kizaramo ambao walikua
wakiongozwa katika misingi ya Sultani Majid na baadae mwaka 1870 Sultan
Barghash.
![]() |
misheni (kanisa) lililotumiwa na viongozi wa kikatoliki kuhifadhi watoto walio nusurika katika bisahara ya utumwa, pia walipatumia kwa kusalia, na kufundishia. |
Awali
misheni hii ilianzishwa kwa lengo la kuwahifadhi watoto walio okolewa katika
biashara ya utumwa, lakini baadae ilikua kubwa na kugeuka kua kanisa, shule na
sehemu ya kufanyia kazi za mikono pamoja na shuguli za kilimo.
Bagamoyo
ndio mji pekee kutembelewa na watafiti wa kwanza kutoka mabara ya ulaya Katika
karne ya 19, ambapo ilikua ndio mwanzo kwa misafara ya Livingstone na wengine.
Kwani mji wa Bagamoyo Haukuwa tu kituo cha biashara kwa ajili ya watumwa na
bidhaa za biashara (pembe za ndovu au Nguta, ambayo ilivunwa kutoka katika nazi
na ilitumika kwa ajili ya utengenezaji wa sabuni) au kituo cha kutengeneza
mashua, lakini ulikua ndio mwanzo wa ujio wa wavumbuzi na watafiti kutoka
ulaya.
Walikua
wakitoka nje ya mji wa Bagamoyo wakitafuta chanzo cha ziwa Nile na maziwa
mengine amabyo yalikua hayaja gunduliwa kwa wakati ule.
Kati
ya walioanza safari yao kutoka Bagamoyo alikua ni livingstone, burton, speke
ambao walikwenda pamoja na Grant kutatua siri za chemchem za mto Nile. Grant
pamoja na Stanley ambao walivunja uhusiano wao katika miaka ya 1871 na
mabaharia 192 na tani 6 ya vifaa, katika kusaka Livingston iliopotea. Na
baadaye tena mwaka 1889 wakati yeye anarudi kutoka miaka 3 ya msafara na
wafanyakazi wake, idadi ilikua imepungua kutoka 708 mpka 196.
Bagamoyo
pia ikawa maarufu kupitia kurudi kwa Livingstone: Baada ya safari ya miezi 9
kutoka Zambia, msiidizi wa livingstone kutoka zanzibari Abdullah Susi na James
Chuma walileta maiti yake ilio kaushwa mjini Bagamoyo mwezi wa pili mwaka 1874.
Mji
wa Bagamoyo unajivunia kuwa na makabila mbalimbali ikiwemo Zaramo na Doe,
Shomvi Waislamu kutoka Oman, hindu kutoka India pamoja na waislamu wengine
kutoka Zanzibari. ambao kwa pamoja wanaishi kwa amani na ushirikiano katika
maisha ya kila siku.
Bagamoyo
umekua kivutio kikubwa sana kwa watalii kutoka nje ya nchi kutokana na maajabu
mengi au historia kubwa ilio kua nayo katika suala ya watumwa pamoja na
uanzilishwaji wa udini.
Mji
ambao umezungukwa na hoteli kubwa na za kifahari kwaajili ya wattalii, wageni
pamoja na wazawa ambao wangependa kuchukua nafasi kuitembelea na kujifunza
mambo mengi ya nyakati za kale kama sehemu moja wapo ya kujua jinsi gani wazee
wetu wa zamani waliishi.
No comments:
Post a Comment